AGRA YAWAFUNDA VIJANA NA WANAWAKE KIBIASHARA MIPAKANI,YAWAPA MBINU ZA KIBIASHARA ILI KUNUFAIKA NA BIASHARA ZAO KIMATAIFA!


Na Joseph Ngilisho ARUSHA 

WANAWAKE na vijana  wanaojishughulisha na uuzaji wa  bidhaa maeneo ya mipakani  wametakiwa kuzalisha bidhaa zenye  ubora ili waweze kushiriki kikamilifu  katika soko huru la Afrika linalolenga  kuwakwamua kiuchumi.  


Aidha katika kukabiliana na vikwazo  visivyo vya kiforodha  wanavyokumbana navyo, sekta ya  umma na sekta binafsi imekutana na  vijana na wanawake wanaofanya  biashara za mazao ya vyakula  mipakani na namna ya kushughulikia  vikwazo visivyo vya kiforodha  .

Hayo yamesemwa jijini hapa leo Ijumaa Machi  28, 2025 na Afisa biashara mkoa wa Arusha, Njivaine Mollel wakati akifungua mafunzo ya majadiliano uliohusisha vijana  zaidi ya 100 kutoka mikoa ya Arusha  na Manyara, wanaofanya biashara  mipakani.  

Aliwataka Wafanyabiashara hao kushiriki mafunzo ya namna hiyo yanayotolrwa na AGRA ili kuwajengea uelewa wa kufanya biashara mipakani na kutumia fursa hiyo ukizingatia kwamba  nchi wanachama wa jumuiya ya afrika mashariki  zimeondoa vizuizi.

Naye Mkurugenzi wa TCCIA ,Oscar Kissanga amesema kuwa,mjadala huo unalenga kuongeza ushiriki wa wafanyabiashara wakina mama na vijana wa bidhaa za kilimo (mahindi ,mchele,maharage,soya,matunda na mbogamboga)ili kuongeza kiwango cha biashara ya mipakani katika bidhaa hizo .

Alisema lengo la majadiliano hayo ni  kuinua vijana na kuwapa elimu,  ikiwemo za kutambua na kukabiliana  na vikwazo pindi wanapofanya  biashara zao kwa lengo la  kuwahamasisha wachangamkie fursa  zilizopo kuanzia soko la ndani hadi la  Afrika.  


"Lengo ni kuhakikisha makundi haya  yanapata fursa ya kujua biashara gani  anaweza kufanya na kwa wakati gani  vikwazo atakavyokutana navyo na  namna ya kukabiliana navyo"


"Tujiandae kuhakikisha hili soko  linalokuja tunazalisha bidhaa zenye  viwango ili tuweze kuuza bidhaa na  kukua kiuchumi," ameongeza

Awali, Ofisa Programu kutoka shirika  lisilo la kiserikali la Aggra, Donald  Mizambwa alisema mjadala huo  unafanyika kupitia program ya Youth  Entrepreneuship for the Future of  Food and Agriculture (Yeffa) ambao  wanashirikiana na Serikali na wadau  wengine kuhakikisha wanaleta  maendeleo kwenye sekta ya kilimo. 


 Alisema kupitia programu hiyo  vijana wenye umri kati ya miaka 18  hadi 35 wanaofanya biashara katika  sekta ya kilimo ikiwemo wanaofanya  maeneo ya mipakani kutoka mikoa 18  nchini wananufaika na program hiyo  ili kutambua fursa za kiuchumi  zilizopo  


Alisema wameungana na Serikali na  wadau wengine kuboresha mazingira  ya kufanyia biashara katika mipaka ya  mikoa ya Mbeya, Songwe, Kigoma,  Kagera, Shinyanga, Mara na Arusha  kwa kupunguza vikwazo visivyo vya  kiforodha.  


Alifafanua  kuwa,Programu hiyo ilianza julai , 2024 katika kipindi hicho hadi sasa wameshafikia vijana 140,000 ambao wamepata zile fursa zilizopo kwenye kazi na  bado kazi inaendelea huku lengo likiwa  ni kufikia vijana 261,000 ambao wamepata fursa za kufanya kazi kwa kipindi cha miaka mitatu .


Alisema kuwa ,Shirika la AGRA ni shirika lisilo la kiserikali ambalo linashirikiana na serikali pamoja na wadau wengine  wa maendeleo katika kuhakilisha kuwa wanaleta maendeleo kwenye sekta ya kilimo .


Alisema kuanzia mwaka 2020/24 AGRA kwa kushirikiana na serikali wanatekeleza mradi unaojulikana kwa jina la EFFA mradi unaofadhiliwa na Mastercard Foundation kwa kushirikiana na AGRA pamoja na wadau wengine wa maendeleo .


“Takribani wiki tatu sasa hadi wiki nne walikuwa wanafanya midahalo  pamoja na  wadau wa serikali na vijana katika kuangalia ushiriki wa vijana katika sekta ya kilimo kwani mradi huo lengo lake ni kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo kwani  kwenye kilimo kuna fursa mbalimbali ikiwemo biashara za mipakani hivyo kwenye mdahalo huo kuna wale vijana wanafanya biashara za mipakani lakini wengine  hawafanyi ila wanatamani kufanya hizo biashara “Alisema


"Lengo ni kuona vijana wanapata fursa  zilizopo sekta ya kilimo lengo mradi ni  kuhakikisha asilimia 80 ni vijana wa  kike kwani kwa tamaduni nyingi  wanawake wanasahaulika na  kuoneakana ni wa kufanya shughuli za  nyumbani, wakati wanaweza kufanya  shughuli za kiuchumi ndiyo maana  tunawashirikisha hapa," Alisema  

Mmoja wa washiriki kutoka mkoani  Arusha, Vanessa Paul, amesema  mafunzo hayo yatawasaidia hasa  vijana wa kike kutambua zaidi fursa  zilizopo na namna ya kuzitumia katika  kukuza uchumi na kuondokana na  utegemezi. 

Tunashukuru mjadala huu  umetuelimisha masuala mengi  ikiwemo kutambua fursa zilizopo nje  ya nchi lakini namna ya kuripoti  vikwazo vya kibiashara pale  tunapokutana navyo na tunaamini  tukiwekeza kwenye kilimo tutakuza  uchumi wetu binafsi na wa taifa kwa  ujumla,"' Alisema







Ends.....

Post a Comment

0 Comments